TAARIFA: Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa leo, Agosti 9, 2022 amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo. Dkt, Hassan Abbasi kumpangia majukumu mengine Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Bw. Godon Nsajigwa.
Taarifa iliyotolewa na Dkt. Abbasi inasema kuwa Meneja huyo anapangiwa majukumu mengine kwa kushindwa kusimamia matumizi endelevu ya Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Akieleza utekelezaji wa agizo hilo, amesema tayari taratibu zimekwishaanza za kupangiwa majukumu mengine na nafasi hiyo inatarajiwa kujazwa mara moja.
Source: #KitengeSports
Post a Comment
Post a Comment