BRUNO Gomez, ni mingoni mwa wachezaji ambao wapenzi wa Yanga walitamani kumuona kikosini mwao msimu huu, chanzo changu ndani ya Singida FG, kimefunguka kuwa pamoja na watu wa Yanga kumtamani Bruno, lakini Mbrazil huyo hakubaliki na uongozi wa juu pamoja na makocha wao.
“Kuna viongozi wa juu kabisa Yanga hawamkubali Bruno. Wanasema bado anahitaji muda zaidi wa kukomaa kumudu kucheza Yanga japo wanaukubali uwezo wake. Nadhani hata makocha (wa Yanga), hawamkubali sana ndio maana hukuona nguvu ikiwekwa kumsajili,”
Kocha wa Singida, Hans van der Pluijm alipoulizwa iwapo kiungo huyo ana nafasi katika kikosi cha Yanga, alisema: “Bruno ni mchezaji mzuri, ila bado anahitaji kukua zaidi kuweza kuhimili kucheza Yanga. Kuchezea Yanga au Simba si kitu kidogo, kule unahitaji uwe umekomaa hasa kuweza kukabiliana na presha za mchezo na mashabiki. “Kule Yanga anaweza kukosea mara moja, mara mbili, mara tatu... mashabiki wakamzomea na kumtoa kabisa mchezoni, hivyo anatakiwa kubaki hapa (Singida) ili aendelee kukomaa zaidi.
.
.
.
Post a Comment
Post a Comment